verse
Maana matendo yako ni mengi sana
Ishara zako Baba ni nyingi mno
Maana wewe ndiye Mungu wangu
Uliniumba niseme matendo yako
Wewe ndiye Mungu, wa miungu eh haleluya baba
Wewe kimbilio letu na ngome yetu
verse
Maneno ya kusema yananikosa
Maana matendo yako ni ya ajabu
Maana ishara zako ni nyingi mno
Kwa macho nimeona makuu yako
Masikio nimesikia matendo yako
Ya kwamba niliumbwa nikuabudu
Mungu wa milele haleluya oh
verse
Mataifa yote ya dunia njoo tumuimbie bwana
Maana fadhili zake ni za milele
Daudi anasema hata wakati moyo wangu unakuwa na uoga
Ni kwako mungu ninajileta
Maana hakuna aliyekutumainia akapata haya
chorus
Haleluya, yesu ni mfalme (Uliniumba nikuabudu)
Uliniumba nikuabudu (oh Uliniumba nikuabudu)
Mataifa yote munisikie haleluyah (oh Uliniumba nikuabudu)
Pasipo yesu mimi singelikuwepo (oh Uliniumba nikuabudu)
Kama si yesu singeliishi oh (Uliniumba nikuabudu)
Wewe ni mwamba wa maisha yangu oh (oh Uliniumba nikuabudu)
Umeokoa wazazi wangu baba (oh Uliniumba nikuabudu)
Umeokoa taifa lako yea(oh Uliniumba nikuabudu)